Dkt. Zarau Kibwe Mkurugenzi Mpya Benk ya Dunia
- nzalinextlevel
- Oct 26, 2024
- 1 min read
Benki ya Dunia imemchagua Mtanzania, Dk. Zarau Kibwe, kuwa Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo atakayesimamia Kanda Namba Moja ya Afrika inayojumuisha nchi 22 ikiwemo Tanzania, nafasi ambayo Tanzania imewahi kuihudumu miaka 54 iliyopita.
Uamuzi wa Dk. Kibwe kuipewa nafasi hiyo nyeti katika Taasisi hiyo kubwa ya Fedha Duniani, umetangazwa katika Mkutano wa Mwaka wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Benki ya Dunia, uliofanyika Jijini Washington D.C, nchini Marekani ambapo mikutano ya mwaka ya Shirika la Fedha Duniani IMF na Benki ya Dunia inafanyika.
Kabla ya kuchaguliwa katika nafasi hiyo, Dk. Kibwe, alihudumu katika Ofisi hiyo ya Bodi kama Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Mshauri na Mshauri Mwandamizi kwa zaidi ya miaka saba, tangu mwaka 2017.

Opmerkingen